Durant Avunja Uhusiano Wake na Russsell Westbrook



Kevin Durant amejitenga na swahiba wake Russell Westbrook baada ya kuigura Oklahoma City Thunders

Mshambulizi mpya wa klabu iliyomalia katika nafasi ya pili katika ligi kuu ya mpira wa vikapu Marekani New Golden State Warriors Kevin Duran amesema kuwa uhusiano wake na mchezaji mwenza wa zamani wa klabu ya Oklahoma City Thunder Russell Westbrook hautasalia tena kuwa kama zamani na itambidi kuzoea mazingira hayo. 

Akizungumza na Shirika la habari la Sina Sports Durant amesema kuwa alizungumza naye Westbrook kabla ya kutia saini kandarasi ya miaka miwili na Warriors. Sasa itambidi Durant kumenyana na mawiji wengine katika kikosi kilichosheheni mastaa wengine akiwemo mchezaji bora NBA msimu uliopita Steph Curry, Klay Thompson na Dreaymond Green hili kujihakikishia nafasi katika kikosi cha kwanza.  

Nilizungumza naye na nikamwelezea mawazo yangu.’’

"Kijumla ni kwamba mahusiano yangu naye hayatasalia kama zamani. Nilizungumza naye na ni matumaini yangu kuwa ataheshimu maamuzi niliyoyafanya.’’

Pia Durant anasisitiza kuwa jambo kuhusu Warriors kubandikwa jina la maadui halimbabaishi kabisa. 

"Kwangu itaniwia vigumu katika hatua za mwanzo kwani sijazoea kumulikwa na umati mkubwa kama sasa. Lakini natumai kuwa nitazoea. Watu wengi hawanipendi hivi sasa na bila shaka wana sababu zao. Naamini kuwa jukumu langu ni kutekeleza majukumu yanayoambatana na wajibu wangu kwa sababu siwezi kufurahisha kila mtu. 

Sasa Kevin Durant anaamini kuwa jukumu lake kuu litakuwa kuisaidia Golden State Warriors katika harakati za kuwinda taji la ligi ambalo walilipoteza baada ya kupepetwa na Cleveland Cavaliers katika fainali kuu msimu uliopita.

Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment