Msahau Draxler: Wenger Aambiwa



Julian Draxler akisherehekea bao katika mchuano wa siku za nyuma

Klabu inayoshiriki ligi kuu Ujerumani Wolfsburg imetengaza kuwa kiungo wake Julian Draxler hataruhusiwa kuondoka Mercedes Benz Arena msimu huu. 

Habari hizi bila shaka ni bonge la kigongo kwa klabu ya ligi kuu Uingereza Arsenal ambayo inasemekana kuwa ilikuwa tayari kupeleka ombi la kumnyakuwa kiungo huyo. 

Wolfsburg ilimaliza nje ya timu zinazoshiriki ligi kuu mabingwa barani ulaya katika ligi ya Ujerumani Bundesliga na kisha mkurugnzi wake mkuu Klaus Allofs akafichua kuwa klabu hiyo ilikuwa radhi kumwuza kiungo huyo ambaye zamani alisakatia Shalke 04. Kwa sasa Draxler amesalia na muda wa miaka minne katika kandarasi yake huku Wolfsburg ikiitisha kitita cha pauni milioni 55 kutoka kwa klabu yoyote inayopania kumsajili kabla ya mkataba wake kutamatika. 

Sasa Allofs amegeuka kinyonga na kusema kuwa sasa Julian hauzwi tena.

"Julian haondoki hapa hata kwa jinsi gani. Nina uhakika kuhusu hilo kwa asilimia 100," Allofs alinukuliwa na kituo cha habari cha Sport1.

"Hakuna mjadala kuhusu hilo."

Arsenal iko katika hali ya hati hati ya kumtafuta msaidizi wa Olivier Giroud katika safu ya ushambulizi baada ya kuzikosa huduma za Jamie Vardy kutoka Leicester. 

Kabla ya kutua Wolfsburg Draxler alihusishwa pakubwa na kuhamia Arsena mnamo mwaka 2013 lakini ikamsajili Mesut Ozil badala yake.

Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment