Giggs Kuondoka Old Trafford



 
 

Kaimu meneja wa Manchester United Ryan Giggs atagura klabu hiyo ikiwa Jose Mourinho atateuliwa kufundisha klabu hiyo msimu ujao. Wakati huo huo idadi ya tiketi za msimu zinazonunuliwa imeongezeka licha ya klabu hiyo kusajili matokeo duni msimu huu.

Giggs anahisi kuwa hatakuwa na uhusiano mwema na Mourinho

Meneja wa klabu ya ligi kuu Uholanzi Ajax Amsterdam Frank de Boer ameonyesha nia ya kujiunga na miamba wa ligi kuu Uingereza Everton msimu kesho. Hii ni kwa mujibu wa wakala wake. Haya yanajiri huku shinikizo za kumuondoa meneja wa sasa Roberto Martinez zikizidi kushika kasi. Robbie savage pia anahisi kuwa mkufunzi wa Newcastle Rafa Benitez anafaa kuridhi mikoba ya Martinez huko Liverpool.

Mchezaji bora msimu nchini Uingerza Riyad Mahrez aliye na umri wa miaka 25 atakataa ombi la pauni milioni 40 la klabu za Arsenal, Barcelona na  Paris St- Germain ili kusalia na mabingwa wa ligi kuu Leicester City.

Leicester pia wanajiandaa kumnunua mshambulizi wa Pescara Gianluca Lapadula, ambaye amefunga mabao 24 msimu huu katika ligi ya daraja la pili Italia Serie B.
Wakati huo huo meneja msaidizi wa Leicester Steve Walsh ambaye pia ni mkuu wa kitengo cha ununuzi wa wachezaji, ametia saini mkataba mpya ili kuendelea kuhudumia mabingwa hao wapya wa ligi kuu Uingereza.

 
 Wachezaji Leicester City wakisherehekea ushindi wa ligi kuu
Maelfu ya mashabiki wa Manchester City hawakuhudhuria hotuba ya mwisho ya meneja wa klabu hiyo anayeondoka Manuel Pellegrini baada ya kusajili sare ya 2-2, hali ambayo huenda ikawafanya City kukosa kumaliza ndani ya nne bora msimu huu.

Mmiliki wa Manchester City walimkabidhi Sheikh Mansour alimkabidhi Manuel Pellegrini mchr halisi wa  LS Lowry kama zawadi ya kuondoka kabla ya kumpisha Pep Guardiola msimu kesho. 

El engeniero atampisha Guardiola msimu ujao
Aitha Pellegrini aliye na umri wa miaka 62 anasema kuwa klabu hiyo imeimarika chini ya uongozi wake licha ya uwezekano wao wa kushiriki Champions Lague msimu ujao kukumbwa na hati hati.

Kiranja wa Manchester City Vincent Kompany aliye na umri wa  30 atakuwa nje ya dimba hadi msimu ujao kwa sababu ya jeraha. 

Guardiola ataridhi mikoba ya Pellegrini msimu ujao

Chelsea itarejea Everton na ofa ya pauni milioni 40 kwa ajili ya kumnyakua mlinzi John Stones aliye na umri wa miaka 21. Everton wanasisitiza kuwa lazima Chelsea watoe ofa ya pauni milioni.

Klabu hiyo inayochezea michuano yake ya nyumbani katika kiwara cha Stamford Bridge imeanza kukumbwa na masaibu baada ya meneja wake mpya Antonio Conte kukatazwa kuambatana na wasaidizi wake wawili.

 
Chelsea wanapania kuziba pengo litakaloachwa na John Terry kwa kumsajili John Stones. 

Kiranja wa muda mrefu wa klabu hiyo John Terry  anatarajiwa kuondoka mwisho wa msimu huu.
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment