Payet Awazawadi Nyundo



 Nipo Tena Sana: Payet
Dimitri Payet akisherehekea ushindi wa klabu yake ya Westham msimu uliopita.
    Na  Dan Ogega
 
Klabu inayoshirki ligi kuu nchini Uingereza Westham United imepiwa jeki katika harakati zake za za kufanya vyema msimu ujao baada ya mchezaji wake mbunifu mfaransa Dimitri Payet kukariri kuwa kamwe hatahamia kwingine katika msimu wa joto. Hili linajiri baada ya uvumi kuenea kuwa mabingwa wa klabu bingwa barani Ulaya msimu jana Real Madrid walikuwa tayari kupeleka toleo kubwa kwa ajili ya kumnasa mchezaji huyo. 

Payet alifana sana katika dimba la taifa bingwa barani Ulaya lililoandaliwa nchini mwao Ufaransa hali ambayo ilikolesha wino tetesi kuwa huenda miamba wa soka barani humo kama Real Madrid, Juventus na Man Unites wangefukuzia saini yake.

Hapo awali mmiliki mwenza wa timu hiyo David Gold alikuwa ameweka bayana kuwa klabu yoyote ambayo ilikuwa na nia ya kumnasa mfaransa hiyo lazina ingetengana na kitita kisichopungua pauni milioni 50.
Lakini licha ya tumbojoto hili wafuasi wa nyundo wana kila sababu ya kutabasamu baada Payet kudhibitisha kuwa kamwe hatong’atuka klabuni humo na yuko tayari kuwakilisha Westaham katika kampeini yake ya kwanza katika uwanja wake mpya wa Olympic jijini London msimu kesho.

“Nina habari kuhusu klabu kubwa kutaka huduma zangu lakini kwangu hiyo ni ishara ya watu kutambua kazi nzuri ninayoifanya," alisema Payet.

"Kwangu jambo la msingi ni kuwa ninaienda sana West Ham. Msimu jana tulikuwa na mafanikio makubwa na natumai mambo yatakuwa mazuri msimu kesho kwa sababu tutachezea mechi zetu za nyumbani katika uwanja mpya. 

“Nina uhakika asilimia 100 kuwa siendi popote, nina mapenzi ya dhati kwa klabu hii na huu ndio ujumbe wangu kwa wananyundo wote.”

Aidha hii ndio kauli ya mmiliki mwenza wa klabu hiyo Gold ambaye hapo kabla alikuwa amehapa kufanya kila jambo hili kuhakikisha kuwa mchezaji huyo anasalia na wananyundo msimu kesho


Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment