Mbona Wachezaji Hufariki Uwanjani?



 
   Na Dan Ogega

   Mchezaji wa timu ya taifa ya Cameroon Patrick Ekeng amekuwa wa hivi punde kupoteza maisha yake uwanjani akicheza baada ya kuzimia, jambo ambalo limeibua mawimbi ya hofu kuhusu usalama wa afya za wachezaji kutokana na mazoezi wanayoyafanya. Mwingine aliyeponea kifo kwa tundu la sindano ni kiungo wa zamani wa klabu ya Bolton Wanderers Fabrice Muamba, ambaye alizimia kwa muda wa masaa 72 kabla ya kuudiwa na fahamu, huku daktari ake akimshauri kuachana na uchezaji baada ya kupona kabisa. 

 
Fabrice Mwamba alilazimika kutundika daluga zake baada ya kuzimia uwanjani
 
  Takwimu zinapendekeza kuwa angalau wachezaji sita wamepoteza maisha yao kwa muda wa miaka mitatu iliyopita kutokana na ugonjwa wa mshtuko wa moyo. Pia ni nadra kuwa mwaka mmoja kupita bila ya kisa cha mwanariadha wa masafa marefu kuripotiwa kuaga dunia kutokana na maradhi ya yaya haya. 

Habari kama hizi bila shaka hututia hofu kwa kuwa huashiria mwisho wa maisha ya mwanaspoti ambaye alikuwa na maazimio makubwa ya kuleta ufanisi katika taifa lake na pia familia. Jambo lililo bayana ni kuwa sio wachezaji profeshenali pekee ambao hukumbwa na misiba sampuli hii bali pia wale ambao wanajikuza kwa namna fulani. Ropiti za afya zinasema kuwa mwanaspoti yeyote anayefanya mazoezi mazito kuliko kimo chake yuko hatarini kuadhirika na maradhi ya mshtuko wa moyo. 

 Patrick Claude Ekeng Ekeng akizimia uwanjani
  “Wengi wa wanamichezo hasa wa kiume hufariki kutokana na vyanzo vinavyojulikana na kila mtu,’’ anashauri Eric Larose ambaye ni daktari wa moyo na mapafu katika hospitali ya Quebec nchini Canada. 

  Anazidi kuelezea kuwa idadi kubwa ya visa hivi ingeepukwa iwapo waathiriwa wangefahamu hatari na ishara za maradhi ya mshtuko wa moyo. 

  Daktari mwingine Chris Woollam wa mbio za Mississauga Marathon na Toronto Marathon anahoji kuwa vifo vinavyotokea katika mbio za masafa marefu ni vya ajali tu, ingawa uwezekano wavyo kutokea ni wa chini mno kwa waandalizi wa mashindano hayo kuweka mikakati ya kuwakagua wanariadha husika. Ripoti ya utafiti iliyochapishwa katika jarida la matibabu la New England Makala a mwezi Januari ilibainisha kuwa kati ya wanariadha takriban milioni 10.9 walioshiriki mashindano mbali mbali ya riadha katika yam waka 2000 na 2010, 59 walikuwa wanaugua maradhi hayo, hii ikiwa ni asilimia 0.54 ya washiriki wote.
 
  Mmoja kati wa wanamichezo waliofikwa na mauti wakiwa nyugani

 Asilimia kubwa iliwajumuisha wanaume maradhi ya mshipa ya moyo ikiunga sehemu kubwa ya visa hivyo.

Pia hakuna uwezekano wa vifo vya ghafla kutokea miongoni mwa wanariadha ikilinganishwa na idadi kamili ya watu.

 “Kwa sababu hii hakuna vigezo vilivyowekwa  ili kuwakagua wanariadha kabla ya mbio. Hali hii huwaachia jukumu la zito na kung’amua ikiwa wako salama kukimbia au la.''…itaendelea…
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment