Djilobodji Awaokoa Bremen




Mchezaji wa Chelsea Pappy Djilobodji akiichezea Weder Bremen.

      Na Dan Ogega
    Mchezaji wa klabu ya Chelsea anayechezea klabu ya ligi kuu Ujerumani  Bundesliga Werder ameisaidia klabu hiyo kuhepa shoka la kushuswa daraja baada ya kuwafungia bao la ushindi katika mchuano wao wa mwisho msimu huu.

Licha ya bao hilo la dakika ya 88 kushukiwa kuwa lilifungwa wakati mchezji huyo akiwa ameotea, liliisaidia klabu hiyo kusalia katika ligi ya dara la kwanza huku wenzao Eintracht Frankfurt wakishushwa daraja.

Ushindi huo uliiwezesha Weder kuchupa hadi nafasi ya 13 huku Frankfurt wakilazimika kucheza mchujo wa mikumbo miwili dhidi ya Nurnberg ili kung’amua ikiwa watacheza Bundesliga msimu ujao. 

Wakati huo huo mabingwa wa ligi kuu Ujerumani mwaka 2007 VFB Stuttgart walishuka daraja moja kwa moja na wakijiunga na Hannover 96 ambao watacheza ligi ya Bumdesliga 2 msimu kesho.

Djilobodji alikuwa sajili wa mwisho wa Jose Mourinho kabla ya kupigwa kalamu mnamo mwezi Disemba licha ya mreno huyo kusema kuwa hakuwa na habari kuhusu dili hiyo.

 
 Djilobodji baada ya kutia saini kandarasi Chelsea 
Aitha alicheza mara moja akiwa ndani ya jezi ya Chelsea kabla ya kuhamia Bremen kwa mkopo mnamo Januari.

Werder Bremen walikuwa katika nafasi ya 16 wakat wa mjo wake ikiwa ni nafasi mbili na alama mbili nyuma ya Frankfurt when Djilobodji.
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment