Picha Ghettoradio
Na Dan Ogega
Kushushwa
daraja kwa klabu ya Shabana siku chache tu baada ya uongozi mpya wa shirikisho
la soka nchini FKF kuingia ofisini, kulimushtua kila mshikadau katika soka ya Kenya.
Hii ni kwa sababu klabu hiyo ilimaliza katika nafasi ya 10 msimu uliopita
katika ligi kuu ya FKF jambo lililopelekea uongozi wa klabu hiyo kupitia katibu wake Peter Omwando, kukata rufaa kwa jopo la
utatuzi wa mizozo ya masuala ya michezo. Aitha jopo hilo liliamua kuwa
mazingira ya kushushwa kwa klabu hiyo yalikuwa ya utata na namo tarehe 19 mwezi
Aprili likaamua kuwa klabu hiyo irudishwe mara moja kushiriki mechi za ligi ya
dara la pili. Ni bayana kuwa haya ni kinyume cha matarajio ya uongozi wa FKF.
Shabana
hawakua timu pekee iliyosombwa na dhoruba la kushushwa daraja. Klabu ya Hema moja FC inayoshiriki ubingwa wa divisheni
ya kwanza katika Zone B 2 iliyokuwa imeteremshwa daraja licha ya kumaliza
katika nafasi ya sita ilirejeshwa pia baada ya maamuzi la jopo hilo
Aitha vyuma vya vilabu vya Busia
United na Lubinu Rangers bado havijaauniwa huku vikiendelea kusistiza kuwa
hakuna sababu tosha za kushushwa kwao. Kulingana na katibu Jackson Makokha
klabu ya Lubinu Rangers ilimaliza kileleni mwa divisheni ya keanza Zone B1 lakini
wakanyimwa fursa ya kushiriki ligi kuu divisheni ya kwanza. Busia United nayo
walimaliza wa nne lakini wakashushwa daraja badala ya kupandishwa ngazi.
Sasa viongoz wa vilabu hivyo wamepanga kuwasilisha
rufaa katika jopo hilo ili kutafuta haki. Maamuzi kam haya yatazidi kupaka tope
nia ya uongozi wa FKF ikiwa jopo hilo litazidi kupata makosa katika maamuzi yake.
0 comments:
Post a Comment