Mbona Soka ya Afrika Imedorora

Hakuna taifa la kiafrika limewahi kuorodheshwa la kwanza duniani na FIFA

  
 Kiranja wa zamani wa Kodivaa Didier Drogba. Picha Getty Images

 Na Dan Ogega

   Ni kawaida siku hizi kuwa mashabiki wengi wa kiafrika wanaweza kutaja majina kamili ya wachezaji wa ligi  kuu za Ulaya na kuelezea kwa undani kuhusu taaluma zao. Lakini dhubutu kuwapa changamoto ya kutaja kikosi cha kwanza cha timu ya taifa au klabu yoyote ya mtaani. Noma. Wengi watababaika na kusema hawana ufahamu au ukibahatika watataja majina mawili au matatu huku pia wakichemsha kuhusu habari za kina kuhusu wachezaji hawa.

Wamiliki wa  vilabu, mashirikisho yanayodhibiti soka na wizara za michezo kote barani Afrika wote wanafahamu kuhusu kudidimia kwa ufuasi wa soka ya nyumbani, hali inayochangiwa na mvuto wa ligi kuu mbali mbali barani Ulaya kama English Premier League, La Liga, Bundesliga, Serie A na French Ligue 1.

Kwa bahati mbaya mifumo iliyobuniwa ya kutanganza soka ya kiafrika na kuvutia mashabiki ambao hutumia muda mwingi kutazama runinga na kufuatilia ligi zilizo mbali na makazi yao bado haijazaa matunda yaliyotarajiwa. Mambo matano yafuatayo yamechangia hali hii.

Idadi ndogo ya mashabiki wakati wa michuano

 

Katika siku za wikendi na wakati wowote kunapochezwa ligi za Ulaya mashabiki ambao zamani walikuwa wakijitokea nyugani kushabikia klabu zao  huwa wanatazama runinga ili wajue timu zao maarufu zinafanyaje, huku wakipuuza timu zao za mitaani. Badala ya kutumia kiasi kidogo cha pesa kuhudhuria michuano ya nyumbani, mashabiki wengi huona ni heri kununua kinywaji na kujumuika na marafiki wakifuatilia hali ya Wilshere, Diego Costa, Martial au Aguero.
Hali hii unavipokonya kipato cha kuuza tiketi vilabu vya mitaani na kuzidi kuvifilisha. Ni bayana kuwa mashabiki hutokea tu wakati wa michuani inayohusisha vilabu vyenye uhasama almaarufu derby au fainali.

Ukosefu wa muda wa kutosha katika vyombo vya habari.

 
Mchuano wa ubingwa wa klabu barani Afrika. Picha Goal.com
 
Kwa sasa ligi za kiafrika  zimekosa udhamini wa maana kutokana na uchache wa mashabiki wanaozifuatilia.

Wakurugenzi wa kampuni mbali mbali wanajitolea kufadhili ligi ambazo ziko na ufuasi mkubwa, hali ambayo huziweka pabaya zile zilizo na mashabiki wachache.

Ligi nyingi barani hazina namna ya kupeperusha michuano yao kutokana na ukosefu wa wadhamini. Nyingi hutegemea michuanO ya awamu za mwisho kama fainali ili kuvutia mashabiki wengi. 

Wachezaji hutamani ligi za majuu.

Ligi kuu Uingereza ni baadhi ya vivutio kwa wachezaji wa kiafrika. Picha Sportslogos.net

Ni ndoto ya kila mchezaji kujiunga na ligi kuu za Ulaya na kuhepa hali duni ya miundo msingi inayokidhiri nyumbani mwao. Tabia hizi huwapelekea kuparamia nafasi za kujiunga na klabu yoyote ile inayoshiriki ligi hizi.
Ni wachache mno huamua kusalia nyumbani kuwaburudisha mashabiki kwa kipato duni. Nani anaweza dhubutu kulaumu uongozi kwa kulipa mapeni machache wakali rasilimali hazipo?
  
Ufadhili Haupo


Hali ya viwanja ni duni
 
Kampuni nyingi za kimataifa hazina nia ya kununua klabu za kiafrika kama wangefanya kule ulaya Asia au Amerika kwa sababu ligi hizi hazina uwezo wa kuzalisha pesa nyingi.
  
Klabu nyingi husumbuka  kupata mikopo kutoka kwa benki ili ziimarishe miundo msingi au kununua wachezaji kwa sababu hazina uwezo wa kulipa hiyo mikopo na riba inayoamatana. Timu hizi hutegemea msaada wa serikali na kipato kidogo cha kuuza wachezaji ili kufanikisha maazimio yao.

Ligi hazijapewa kipaumbele na wahusika wenyewe.

Nyota wa Cameroon Samwel Eto'o ni baadhi ya wacheaji waliohamia ligi za bara Ulaya.

Ni kawaida kuwa taswira kamili ya profeshenali katika soka ni kucheza EPL au La Liga.  Baada ya kupata hela za mishahara, wao ndo hupewa nafasi katika jamii hali inawapelekea kuchukua soka ya nyumbani na kutamani kupata mwanya na kutoroka  nyumbani.
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment