N'Golo Kante Kutua Arsenal.



 
 N'Golo Kante akiwajibikia Leicester City
          Na Dan Ogega
    Huenda klabu ya Arsenal imeamua kutowazingua tena wafuasi wake msimu ujao baada ya kuafikia makubaliano ya kumsajili kiungo mkabaji wa Leicester City mfaransa N’Golo Kante. Habari ambazo zimezagaa katika majarida ya Ufaransa ni kuwa Kante ameridhia kuhamia London msimu ujao. 

Kante ambaye alijumuishwa katika kikosi cha msimu uliopita katika ligi kuu Uingereza baada ya kuisaidia Leicester kushinda taji la Uingereza, anakadiriwa kugharimu Arsenal kitita cha pauni milioni 20. Aitha anasemekana kuvutiwa na mfumo wa meneja Arsene Wenger na pia uhusiano wake mzuri na wacheaji chipukizi. 

Mchezaji huyo amekuwa akihusishwa pakubwa na kuhamia London huku kituo cha televisheni cha French TV kupitia kipindi chaTelefoot kikifichua kuwa uvumi huo huenda ukawa ukweli katika siku za usoni. 

Vyanzo vingine vinasema kuwa wakala wa Kante amekutana na wawakilishi wa wanabunduki hao ili kufuma dili hiyo kikamilifu.

N'Golo Kante pia amehusishwa na vilabu kadhaa vikiwemo Manchester United na Manchester City lakini meneja mpya wa City Pep Guardiola anasemekana kutopendezwa na uchezaji wa mfaransa huyo.

Kante atashiriki michuano ya taifa bingwa bara ulaya na timu ya Ufaransa.


Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment