Matic' Kumfuata Mourinho Old Trafford



 
Nemanja Matic na Jose Mourinho wana uhusiano mwema 
   Na Dan Ogega 
   Meneja Mpya mtarajiwa wa Manchester United Jose Mourinho hatachukua muda mrefu kuimarisha kikosi chake, kwani atavamia kambi ya klabu yake ya zamani Chelsea akizisaka huduma za kiungo mkabaji mserbia Nemanja Matic katika harakati za kwanza za kutumia mtaji wa pauni milioni 200 atakazopokezwa na wamiliki wa Manchester United. Mourinho anapendelea kipaji cha mchezaji huyo ambaye alimrejesha Stamford Bridge kutoka Benfika kuliko wachezaji waliomo kikosini kama Moruane Fellaini na Michael Carrick, ambao wameorodheshwa kama vyanzo vya mashetani wekundu kuchemsha katika siku za nyuma. Inakisiwa kuwa Matic ataigharimu United kitita cha pauni milioni 25.
  
Pia the special one kama anavyojitambulisha mreno huyo atapeleka toleo Everton kwa ajili ya kumnasa mkabaji wao John Stones ambaye anakadiriwa kugharimu kima cha pauni milioni 45, huku pia mkondo wa pili ukimuelekeza Madrid ambapo takriban pauni milioni 35 zitakuwa tosha kumtia kapuni mfaransa Raphael Varane.

Wakati huo huo kiungo wa United Mhuspania United Juan Mata ataandaa mazungumzo na Mourinho ili kumuelezea mreno huyo nia yake ya kusalia Old Trafford, wakati mhispania mwengine kipa David de Gea akikisiwa kujianda kusepa kuelekea Real Madrid.

Katika kipindi chake kama mkufunzi huko Chelsea Mourinho alimponza Mata kabla ya kuamrisha kuuzwa kwake kwenda Manchester United mnamo Januari mwaka 2014 kwa dhamani ya pauni milioni. Vyanzo vya habari kutoka Manchester vinasema kuwa Mata yuko tayari kurudiana na meneja wake wa zamani huku akisistiza kuwa kamwe hajawahi kukosana na Mourinho. 

Hatua ya kumteua Mourinho kama meneja mpya wa klabu ya Manchester United ni jambo la muda tu baada ya Mholanzi Luis Van Gaal kupigwa ufagio wa chuma mapema juma hili. Kitendo hiki kinatarajiwa kuleta mwanzo mpya baada ya uchezaji chwara klabu hiyo imekuwa ikidhihirisha katika siku za nyuma tangu kuondoka kwa kocha wa zamani wa klabu hiyo Mskochi Sir Alex Ferguson.  


Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment