Mbona Neymar atakuwa Bora Zaidi ya Ronaldo na Messi




 

     Na Dan Ogega
Mjadala kuhusu nani bora zaidi kati ya Cristiano Ronaldo na Lionel Messi umetamalaki vyombo vya habari kwa muda mrefu sasa. Wawili hao wameshinda mataji manane ya mchezaji bora duniani kati yao katika muongo mmoja uliopita jambo lililowafanya wengi kuamini kuwa hakuna mchezaji atawahi kuibuka na kuwapiku katika ufanisi huo.



Kando na mjadala huu ambao kamwe huwezi bainisha mbivu na mbichi ni muhimu kuzingatia kuwa kinda mbrazil Neymar Santos ana miaka mingi ya kucheza kabumbu na pia ana talanta na uwezo wa kusawazisha au hata kuwapiku wawili hao.


Akiwa na umri wa miaka 23 Neymar amepachika mabao 183 akichezea vilabu vya Santos, Barcelona na timu ya taifa ya Brazil,hii ikiwa ni kadri ya mabao 0.57 kwa kila pambano

Wakiwa katika umri huo huo Messi alikuwa amecheka na nyavu mara Messi 150 huku Ronaldo akiliona lango mara 118.


Neymar pia yuko mbioni kuvunja rekodi ya kuwakilisha Brazil mara nyingi na pia kuwa mfungaji bora wa vijana wa Samba.


Hadi sasa amesalia kuchezea Brazil mara 76 ndio asawazishe rekodi ya veterani wa taifa hilo Cafu aliyeshuka dimbani mara 142 akiivaa jezi ya Samba na pia akifanikiwa kufunga mabao 31 zaidi atakuwa ameichakaza rekodi ya nguli wa soka duniani Edson Arantes do Nascimento almaarufu Pele katika chati za wafungaji bora Brazil.
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment