Walcott Kuhama Arsenal


  Welbeck amemfanya Walcott Kuhama Arsenali

 

      Na Dan Ogega
   Huenda winga machachari wa Arsenali Theo Walcott akagura klabu hiyo katika soko la majira ya joto baada ya nafasi yake katika kikosi cha kwanza kuwa nadra. Tangu mwezi Januari Muingereza huyo meanza mara moja tu katika kikosi cha kocha mfaransa Arsene Wenger.
 
   Walcott ambaye kwa sasa yuko na umri wa miaka 27 amefunga mara tano  katika michuano 15 aliyoanza lakini kwa sasa anaketisha benchi huku muingereza mwenzake Danny Mensah Welbeck na kinda mnaijeria Alex Iwobi wakianzishwa kila mara 

   Pia uwezekano wake kuunda kikosi cha timu ya taifa ya uingereza kitakachoshiriki michuano ya taifa bingwa barani ulaya mwaka huu imekumbwa ta sintofahamu baada ya meneja wa timu hiyo Roy Houghson kusema kuwa itabidi atie bidii zaidi.

   Kaimu meneja wa zamani wa klabu ya Chelsea Ray Wilkins anahisi kuwa atahitajika kugura washikabunduki hao wa London ili kuendelea kuchezea Uingereza.

 "Mambo sio mazuri kwa Walcott  ikiwa ataendelea kulikamua benchi la klabu ya Arsenali katika kiwango hiki katika taaluma yake. Kwa sasa anahitajika kucheza kila mara.  

"Kwa sasa yuko kweye mtanziko kwa sabau hataweza kuinga kama mshambulizi wa kwanza katia klabu yake . Kama anataka kucheza kama straika basi mstakabali waake haupo klabuni arsenali."

Walcott alijiunga na Arsenali mnamo mwaka 2006 akitokea klabu ya Southampton.


Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment