Spurs Hawatashinda EPL: Hazard



Nyota wa Chelsea Eden Hazard awaonea kijicho Tottenham 

 

          IMG_8400.JPG 
      Na Edwin Mwangi
Kiungo wa kati wa Chelsea Eden Hazard  amesema kwamba yeye na wachezaji wenzake hawaitakii Tottenham kushinda ligi kuu Uingereza. Spurs wako alama nane chini ya Leicester huku zikibakia tu mechi nne pekee.

Chelsea ambao ni mabingwa watetezi  wanachuana na mahasimu wao wa jadi wa jiji la London  Spur nyumbani tarehe 2 mwezi ujao na kisha kufunga virago na kisha kupungia mkono kikombe mkono wakicheza na Leicester 15 May, mechi ya mwisho ya msimu huu.

" Mashabiki, klabu na wachezaji hatutaki Tottenham washinde ligi, "  Hazard, 25, alinukuliwa na BBC
"Tunawatakia Leicester kila la heri kwa sababu wanastahili kuwa mabingwa msimu huu.'' 

"Tuna mchuano mzuri wiki ijayo dhidi ya Tottenham na kama tutawashinda basi ni vyema."

Hazard, Mchezaji bora wa 2015, alifunga mara mbili katika mechi kati yao na Bournmouth Jumamosi wakati Chelsea waliwacharaza Bournmouth4-1 yakiwa ni mabao yake ya kwanza msimu huu.

 
Hazard akikabiliana na Spurs 
 
Kiungo wa kati wa Chelsea  Cesc Fabregas, zamani akichezea Arsenali kuanzia  2003 hadi 2011, pia anaitakia Leicester ushindi na anawataka kutwaa ligi kabla ya mechi yao dhidi ya Chelsea. 

"Nina imani watakuwa wameibuka washindi wakati huo," raia huyo wa uhispania alliambia Sky Sports.

"Spurs wanasukuma sana kuhakikisha wamewapiku Liecester lakini nadhani Liecester watashinda. ”

"Sitaki Spurs washinde na vile wamefanya msimu huu ningependa Liecester wachukue ligi."

Mchanganuzi wa Match of the Day Martin Keown alisema matamshi ya Hazard yatawatia Spurs hasira kabla ya mchuano dhidi ya  Chelsea
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

1 comments: