Mwanasayansi Ashiriki Mbio za London Marathon Akiwa Angani

  
 Time Peake akiwa angani
 
   Eliud Kipchoge aliongoza washiriki takriban elfu 38,000 jana Jumapili katika mbio za London Marathon huku mpinzani mmoja akishiriki shindano hilo akiwa maili 200 juu ya sayari ya dunia. 

    Mwanasayansi muingereza Tim Peake alikamilisha mbio hizo za kilomita 42 au maili 26.2 akiwa katika kituo wanasayansi cha International Space Station kwa muda wa 3:35.21 ,jambo ambalo ni la kwanza kutokea katika historia ya riadha. Haya ni kwa mujibu wa shirika la anga la bara Uropa ESA. 

Bwana Peake ndiye alikwa mwanzilishi rasmi wa mbio hizo huku ujumbe wake wa video ukitumika kung'oa nanga shindano hilo.

Kukimbia angani kuna changamoto lukuki hasa ikizingatiwa kuwa ukosefu mvuto  wa dunia hupelekea mmoja kukosa kuwa na uzani.

  "Wakati tu unaacha kukimbia misuli yako huwa imetulia kabisa na pia kupona kutokana na maumivu huchukua muda mrefu sana." 
Eliud Kipchoge akisherekea ushindi London

Katika mbio hizo Eliud Kipchoge alilitetea taji la wanaume ikiwa ni sekunde nyuma ya rekodi ya dunia baada ya kukata utepe mbele ya kasri ya Buckingham kwa muda wa 2:03:05. Mkenya mwingine Jemima Sumgong alishinda taji la wanawake baada ya kukata utepe baada ya 2:22:05.
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment