Makosa Makubwa Zaidi ya Wenger




 

        Na Dan Ogega 

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Liverpool Jamie Carragher anaamini kuwa hatua ya meneja wa Arsenal Arsene Wenger ya kutomsajili straika wa Barcelona Luis Suarez, ndio makosa makubwa zaidi atakayoyajutia katika taaluma yake. Suarez ambaye ni raia wa Uruguay alikuwa ameridhia kuhamia uwanjani Emirates laini mkono ghamu wa Wenger ukamnyima fursa hiyo.


Msimu uliofuata aliisaidia Liverpool kumaliza katika nafasi ya pili ligini na baadaye akakamilisha uhamisho wa pauni milioni 75 kwenda Barcelona.

Msimu uliopita alibugia mabao 25 huku akiwa tayari ashafunga maradufu ya idadi hiyo msimu huu.
Wakati huo huo Arsenal wanazidi kuchemsha na kusajili matokeo dinu huku mshambuliaji wake mfaransa Olivier Giroud akiwa mfungaji bora kwa baada ya kucheka na nyavu mara 12 katika ligi kuu Uingereza msimu huu. 

"Ukiangazia miaka 20 ya Arsene Wenger katika ligi kuu ya premia Uingereza kuna mengi makubwa ambayo ameyatimiza, lakini mwezi Julai mwaka 2013 hautasahaulika kwa sababu alikosa kushawishi Liverpool kumuuzia Suarez.’’ Carragher aliandikal katika blogu yake katika jarida la Daily Mail.

"Wenger ana rekodi ya kuwa mmakinifu katika matumizi ya pesa kwa sababu yeye hutumia fedha za klabu pale anapohisi kuwa atapata matokeo mazuri. Hii ni ishara ya uhuru wa kungojea na ungojea aliopewa na klabu hiyo.’’

‘Msimu uliopita katika majira ya joto kwa mfano alisajili tu mchezaji mmoja tu ambaye ni golikipa wa Chelsea Petr Cech na akapuuza kusajili kiungo yeyote.’’

"Kama Arsenal wangeshinikiza kumsajili, labda kwa toleo la pauni milioni 50 naamini wangenyakua taji la ubingwa wa ligi kuu Uingereza mara mbili katika misimu mitatu iliyopita. Huo ndio ukweli kumhusu Suarez kwa sabau timu yoyote aichezeayo, yeye huwa vuruta hadi upeo wa juu.’’
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment