Van Gaal Kuondoka United



 

      Na Dan Ogega 
Ushindi katika kome la FA hautakiokoa chuma cha Louis van Gaal kwani atafurushwa mwishoni mwa msimu huu. Haya ni kulingana na kauli ya mwanahabari wa jarida la The Sun Neil Custis ambaye pia anahisi kuwa huendaJose Mourinho akaridhi cheo cha mholanzi huyo katika uwanja wa Old Trafford.

Ushindi wa 2-1 dhidi ya Everton siku ya Jumamosi unamaanisha kuwa sasa mashetani hao wekundu wana nafasi ya kukata kiu ya taji ambayo imedumu tangu mwaka 2013. Mkataba wa Van Gaal ambaye amekosolewa sana katika siku za hivi karibuni baada ya matokeo ya kuvunja moyo unatamatika mwaka huu huku Curtis akihoji kuwa uamuzi wa kumtimua tayari ushafanyika. 

"Nina uhakika kuwa uamuzi ushafanyika kuwa Mourinho atawasili Manchester United msimu ujao.

"Mourinho amenawiri kila mahali ameenda jambo ambalo ni tiketi yake kumrithi van Gaal.
"Sidhani kuwa ushindi dhidi ya Everto utafuta rekodi yake mbaya kwa muda wa miezi 18 iliyopita ambayo kiukweli ni mbovu sana. 

"Kama tungeshuhudia matokeo kama ya jana kwa muda huo basi hatungedhubutu kuuliza kuhusu umilisi wake kufunza United.’’

Licha ya shinikizo la kuleta ufanisi kwa klabu hiyo van Gaal amepewa heko kwa kuwaleta chipukizi katika kikosi chake jambo ambalo limemwauni japo kwa kiduchu. Lakini Curtis anahoji kuwa jambo hilo lilichangiwa na wachezaji wa kikosi cha kwanza kuwa majeruhi.

 "Kuhusu suala la kuwaleta vijana katika kikosi cha kwanza kwangu sio mshangao kwa sababu ya hali ya majeraha. Lisingejiri hatungepata nafasi ya kuwaona kina Marcus Rashford.

"Labda mara moja kwa kila mwezi tuna wakati tunaposema, labda kuna kitu kizuri kinakuja kuna ishara ya maendeleo.’’

"Kwa vyovyote vile chochote kitakachojiri tangu sasa hadi mwisho wa msimu hakitabadili mustakabali wa Van Gaal ."

Jose Mourinho yuko huru kujiunga na United kufuatia kutimuliwa kwake kutoka Chelsea mnamo mwezi Disemba mwaka jana,

United walimaliza katika nafasi ya nne msimu uliopita lakini wakabanduliwa kutoka mechi za klabu bingwa barani Ulaya na pia kwenye kombe la Europa League na mahasimu wa jadi Liverpool katika awamu ya 16 bora.
Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment