Terry ni wa Kulauimiwa kwa Kichapo cha 3-0




 
 Chelsea wachemsha nyumbani
                     Na Edwin Mwangi
 

   Mchezaji wa zamani wa klabu ya Liverpool Graeme Souness amemkashifu kiranja wa Chelsea John Terry kwa kichapo cha Jumamosi dhidi wa Man City ugani Stanford Bridge . Souness anahoji kuwa kuwepo kwa Terry kungezuia kichapo cha 3-0 machoni mwa mashabiki wao wa nyumbani. Mchezaji na straika matata wa City Sergio Aguero alidhihirisha umahiri wake kwa kutia wavuni mara tatu na kudidimiza na kuchafua mchezo wa Chelsea wa kitabu na kumwaacha mkufunzi wa muda Guus Hiddink kuandikisha kichapo chake cha kwanza nyumbani. 
 
   Chelsea walianza mchuano huo kwa kishindo na kutia matumaini mashabiki lakini uwepo wa mchezaji wa zamani wa Wolfsburg Kevin De  Bryune  kuhemesha timu yake ya zamani na kuwaadhibu mabeki na mbio zake za kanga.

Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment