Vipi Man City Watawaangusha Real Madrid?

Real imesheheni nyota lakini City wana nafasi


 
    
     Na Dan Ogega 
Dhana ambayo imeghubika washikadau wa klabu ya Man city ni kuwa wanahitaji kufuzu kwa awamu ya nusu fainali ya kombe la klabu bingwa bara ulaya mara nne au zaidi ndiposa wapate kulinyakua. Hii ni kwa sababu awanu ya maondoano ni karata ya bahati nasibu na hakuna kutegemea majanga ya ghafla kwa klabu kubwa zinazoshiriki dimba hilo.

Mashabiki wa klabu hiyo walifurahia habari kuwa huenda Cristiano Ronaldo hangeshiriki mchuano wa mkumbo wa kwanza hii leo kiwarani Etihad, lakini iwapo atakuwa fiti kucheza basi itabidi wamkabili vilivyo kama wanataka kucheza mechi ya marudiano ugani Santiago Bernabeau mwezi kesho wakiwa na matumaini.

Licha ya zimwi hili linaloikabili Man City ni muhimu kukumbuka kuwa Kamari hii inaweza kugeuza kibao kwa madrid ikiwa wakakosa kuwa katika ubora wao kimchezo. Los Blancos walitinga nusu fainali lca kumfukuza Benitez jambo lililosambaratisha maazimio ya klabu hiyo.
Aliyeridhi mikoba yake mfaransa Zinadine Zidane akizungumza na wanahabari jana alidhihirisha kuwa kuna ushikamano fulani licha ya kuwepo mushkeli kidogo kikosini.

Zizou akiwahutubi wanahabari baada ya kuteuliwa kuwa meneja wa Real Madrid

Mfaransa huyo huleta mchecheto na kuzoa matokeo mazuri. Tangu enzi za kufunza kikosi cha pili cha Madrid yaani Castilla Zidane alikuwa amezoea uhuru wa  kufanya kazi kwa ushirikiano kutoka kwa kila mshikadau. Kikosi kilikuwa kikisafiri kwa basin a pia alikuwa amepewa hela za kusajili wachezaji jambo ambalo ni msamiati kwa meneja wa sasa wa Castilla Luis Miguel Ramos.

Hadi sasa ni bayana kuwa rais wa klabu hiyo Florentino Perez anaamini kuwa Zidane anaweza kuongoza klabu hiyo katika harakati za kufikia upeo mpya, nafasi ambayo imekuwa kama kucheza na shilingi kariku na tundu la msalani. Mameneja kadhaa wamefurushwa akiwemo Jose Mourinho, Carlo Ancelotti na Manuel Pellegrini. Msimu uliopita alimpuuza wakati wa akimnyakuwa Rafa kutoka Napoli huku Zizou akionekana kutoridhishwa na uamuzi huo.
Kwa hivyo hatua ya kujaza pengo la Benitez na Zizou ni uamuzi ambao haukutarajiwa na wengi na ambao haukutarajiwa kuleta mafanikio kaltika klabu hiyo.
 
 Ramos anaripotiwa kutoridhika na maamuzi ya uongozi wa Real Madrid

Nyuma ya pazia la kuuza sera za klabu katika mahojiano ya jana jioni, kuna ulegevu fulani ambao unaonekana katika kikosi chake. Katika michuano mikubwa sampuli ya huu wa leo nyota wao CR7 hutarajia viungo wenzake kama James Rodriquez na Marcelo Vieira kumpitishia mpira na ikiwa watakosa basi yeye hubaki akiteta.

Kila wakati mchezaji ghali Zaidi Gareth Bale hujipata ako pembeni mwa uwanja hii ikiwa ni baada ya lalama za Ronaldo baada ya Bale kujaribiwa kama straika. 

 “Mbona mnamchezesha hapa? Hii ni nafasi yangu.’’ Alibweka CR7
 
Ronaldo akilalamikia hali duni ya wachezaji wenzake uwanjani

Hali ya kujipendelea inaweza kuchipuka katika  mazingira sampuli hii. Msimu uliopita kiranja wa klabu hiyo Sergio Ramos aliitisha kura ya maoni ya ikiwa wangemuondoa daktari wa klabu hiyo baada yake kushukiwa kuwadukua wachezaji katika vyumba vya kubadilisha mavazi.

Ni kikosi kinachosheheni wachezaji wanaopigania umaarufu huku Ramos akiwa mmoja wao. Jambo linaloharibu mambo zaidi ni kuwa alitamani kugura klabu hiyo miezi minane iliyopita. Uhusiano kati yake na Perez ni mgumu kwa wakati huu huku Ramos akidhibitisha kuwa alikuwa amekubali makataa ya kuhamia Manchester United. Alibaki tu ili kuendeleza sera za Perez ambaye ni kero kwa wafuasi wa klabu hiyo.

Ramos pia alisazwa ili kupiga jeki idadi wa wahispania wanaounga kikosi cha kwanza cha klabu hiyo. Kwa maana hiyo, alimkabidhi Ramos mkataba wa kima cha pauni milioni 10 na kuzima uhamisho wa Nicolas Otemendi aliyejiunga na City.
Gareth Bale

Kudhibiti mienendo ya wachezaji wakubwa sio kazi rahisi. Kiujumla ni kuwa muitaliano Ancelotti alijaribu kutekeleza wajibu huu. Labda ni kwa sababu aliwapa uhuru wa kucheza bila shinikizo.

Hali hii ya mshikemshike huenda ikanufaisha City kwani wakitilia maanani vigezo vya uchezaji bora huenda wakawapiku Real usiku wa leo.


Share on Google Plus

Kuhusu Unknown

Michezo Kenya Tunapenda Spoti

0 comments:

Post a Comment